Qurani


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

وَالذَّارِيَاتِ ذَرْوًا
1.
Naapa kwa pepo zinazo tawanya,
فَالْحَامِلَاتِ وِقْرًا
2.
Na zinazo beba mizigo,
فَالْجَارِيَاتِ يُسْرًا
3.
Na zinazo kwenda kwa wepesi.
فَالْمُقَسِّمَاتِ أَمْرًا
4.
Na zinazo gawanya kwa amri,
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَصَادِقٌ
5.
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka ni kweli,
وَإِنَّ الدِّينَ لَوَاقِعٌ
6.
Na kwa hakika malipo bila ya shaka yatatokea.
وَالسَّمَاءِ ذَاتِ الْحُبُكِ
7.
Naapa kwa mbingu zenye njia,
إِنَّكُمْ لَفِي قَوْلٍ مُّخْتَلِفٍ
8.
Hakika nyinyi bila ya shaka mmo katika kauli inayo khitalifiana.
يُؤْفَكُ عَنْهُ مَنْ أُفِكَ
9.
Anageuzwa kutokana na haki mwenye kugeuzwa.
قُتِلَ الْخَرَّاصُونَ
10.
Wazushi wameangamizwa.
الَّذِينَ هُمْ فِي غَمْرَةٍ سَاهُونَ
11.
Ambao wameghafilika katika ujinga.
يَسْأَلُونَ أَيَّانَ يَوْمُ الدِّينِ
12.
Wanauliza: Ni lini hiyo siku ya malipo?
يَوْمَ هُمْ عَلَى النَّارِ يُفْتَنُونَ
13.
Hiyo ni siku watakayo adhibiwa Motoni.
ذُوقُوا فِتْنَتَكُمْ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تَسْتَعْجِلُونَ
14.
Onjeni adhabu yenu! Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyahimiza.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ
15.
Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.
آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ ۚ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُحْسِنِينَ
16.
Wanapokea aliyo wapa Mola wao Mlezi. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema.
كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ
17.
Walikuwa wakilala kidogo tu usiku.
وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُونَ
18.
Na kabla ya alfajiri wakiomba maghfira.
وَفِي أَمْوَالِهِمْ حَقٌّ لِّلسَّائِلِ وَالْمَحْرُومِ
19.
Na katika mali yao ipo haki ya mwenye kuomba na asiye omba.
وَفِي الْأَرْضِ آيَاتٌ لِّلْمُوقِنِينَ
20.
Na katika ardhi zipo Ishara kwa wenye yakini.
وَفِي أَنفُسِكُمْ ۚ أَفَلَا تُبْصِرُونَ
21.
Na pia katika nafsi zenu - Je! Hamwoni?
وَفِي السَّمَاءِ رِزْقُكُمْ وَمَا تُوعَدُونَ
22.
Na katika mbingu ziko riziki zenu na mliyo ahidiwa.
فَوَرَبِّ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ إِنَّهُ لَحَقٌّ مِّثْلَ مَا أَنَّكُمْ تَنطِقُونَ
23.
Basi naapa kwa Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, hakika haya ni kweli kama ilivyo kweli kuwa nyinyi mnasema.
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ ضَيْفِ إِبْرَاهِيمَ الْمُكْرَمِينَ
24.
Je! Imekufikia hadithi ya wageni wa Ibrahim wanao hishimiwa?
إِذْ دَخَلُوا عَلَيْهِ فَقَالُوا سَلَامًا ۖ قَالَ سَلَامٌ قَوْمٌ مُّنكَرُونَ
25.
Walipo ingia kwake wakasema: Salama! Na yeye akasema: Salama! Nyinyi ni watu nisio kujueni.
فَرَاغَ إِلَىٰ أَهْلِهِ فَجَاءَ بِعِجْلٍ سَمِينٍ
26.
Akenda kwa ahali yake na akaja na ndama aliye nona.
فَقَرَّبَهُ إِلَيْهِمْ قَالَ أَلَا تَأْكُلُونَ
27.
Akawakaribisha, akasema: Mbona hamli?
فَأَوْجَسَ مِنْهُمْ خِيفَةً ۖ قَالُوا لَا تَخَفْ ۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَامٍ عَلِيمٍ
28.
Akahisi kuwaogopa katika nafsi yake. Wakasema: Usiwe na khofu, nao wakambashiria kupata kijana mwenye ilimu.
فَأَقْبَلَتِ امْرَأَتُهُ فِي صَرَّةٍ فَصَكَّتْ وَجْهَهَا وَقَالَتْ عَجُوزٌ عَقِيمٌ
29.
Ndipo mkewe akawaelekea, na huku anasema na akijipiga usoni kwa mastaajabu, na kusema: Mimi ni kikongwe na tasa!
قَالُوا كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِ ۖ إِنَّهُ هُوَ الْحَكِيمُ الْعَلِيمُ
30.
Wakasema: Ndivyo vivyo hivyo alivyo sema Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mwenye kujua.
قَالَ فَمَا خَطْبُكُمْ أَيُّهَا الْمُرْسَلُونَ
31.
AKASEMA: Basi ujumbe wenu ni nini, enyi mlio tumwa?
قَالُوا إِنَّا أُرْسِلْنَا إِلَىٰ قَوْمٍ مُّجْرِمِينَ
32.
Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa watu wakosefu,
لِنُرْسِلَ عَلَيْهِمْ حِجَارَةً مِّن طِينٍ
33.
Tuwatupie mawe ya udongo,
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلْمُسْرِفِينَ
34.
Yaliyo tiwa alama kutoka kwa Mola wako Mlezi kwa ajili ya wanao pindukia mipaka.
فَأَخْرَجْنَا مَن كَانَ فِيهَا مِنَ الْمُؤْمِنِينَ
35.
Kwa hivyo tutawatoa katika hao wale walio amini.
فَمَا وَجَدْنَا فِيهَا غَيْرَ بَيْتٍ مِّنَ الْمُسْلِمِينَ
36.
Lakini hatukupata humo ila nyumba moja tu yenye Waislamu!
وَتَرَكْنَا فِيهَا آيَةً لِّلَّذِينَ يَخَافُونَ الْعَذَابَ الْأَلِيمَ
37.
Na tukaacha humo Ishara kwa ajili ya wanao iogopa adhabu chungu.
وَفِي مُوسَىٰ إِذْ أَرْسَلْنَاهُ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ
38.
Na katika khabari za Musa, tulipo mtuma kwa Firauni na hoja wazi.
فَتَوَلَّىٰ بِرُكْنِهِ وَقَالَ سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
39.
Lakini alipuuza kwa sababu ya nguvu zake na akasema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu!
فَأَخَذْنَاهُ وَجُنُودَهُ فَنَبَذْنَاهُمْ فِي الْيَمِّ وَهُوَ مُلِيمٌ
40.
Basi tukamkamata yeye na majeshi yake na tukawatupa baharini, na yeye ndiye wa kulaumiwa.
وَفِي عَادٍ إِذْ أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمُ الرِّيحَ الْعَقِيمَ
41.
Na katika khabari za A'di tulipo wapelekea upepo wa kukata uzazi.
مَا تَذَرُ مِن شَيْءٍ أَتَتْ عَلَيْهِ إِلَّا جَعَلَتْهُ كَالرَّمِيمِ
42.
Haukuacha chochote ulicho kifikia ila ulikifanya kama kilio nyambuka.
وَفِي ثَمُودَ إِذْ قِيلَ لَهُمْ تَمَتَّعُوا حَتَّىٰ حِينٍ
43.
Na katika khabari za Thamudi walipo ambiwa: Jifurahisheni kwa muda mdogo tu.
فَعَتَوْا عَنْ أَمْرِ رَبِّهِمْ فَأَخَذَتْهُمُ الصَّاعِقَةُ وَهُمْ يَنظُرُونَ
44.
Wakaasi amri ya Mola wao Mlezi. Basi uliwanyakua moto wa radi nao wanaona.
فَمَا اسْتَطَاعُوا مِن قِيَامٍ وَمَا كَانُوا مُنتَصِرِينَ
45.
Basi hawakuweza kusimama wala hawakuwa wenye kujitetea.
وَقَوْمَ نُوحٍ مِّن قَبْلُ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا قَوْمًا فَاسِقِينَ
46.
Na kaumu ya Nuhu hapo mbele. Hakika hao walikuwa watu wapotovu.
وَالسَّمَاءَ بَنَيْنَاهَا بِأَيْدٍ وَإِنَّا لَمُوسِعُونَ
47.
Na mbingu tumezifanya kwa nguvu na uwezo na hakika Sisi bila ya shaka ndio twenye uwezo wa kuzitanua.
وَالْأَرْضَ فَرَشْنَاهَا فَنِعْمَ الْمَاهِدُونَ
48.
Na ardhi tumeitandaza; basi watandazaji wazuri namna gani Sisi!
وَمِن كُلِّ شَيْءٍ خَلَقْنَا زَوْجَيْنِ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ
49.
Na katika kila kitu tumeumba kwa jozi ili mzingatie.
فَفِرُّوا إِلَى اللَّهِ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
50.
Basi kimbilieni kwa Mwenyezi Mungu, hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
وَلَا تَجْعَلُوا مَعَ اللَّهِ إِلَٰهًا آخَرَ ۖ إِنِّي لَكُم مِّنْهُ نَذِيرٌ مُّبِينٌ
51.
Wala msifanye kuwa kuna mungu mwengine pamoja na Mwenyezi Mungu. Hakika mimi ni mwonyaji kwenu wa kubainisha nitokae kwake.
كَذَٰلِكَ مَا أَتَى الَّذِينَ مِن قَبْلِهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا قَالُوا سَاحِرٌ أَوْ مَجْنُونٌ
52.
Basi ndio hivyo hivyo, hakuwajia kabla yao Mtume ila walisema: Huyu ni mchawi au mwendawazimu.
أَتَوَاصَوْا بِهِ ۚ بَلْ هُمْ قَوْمٌ طَاغُونَ
53.
Je! Wameambizana kwa haya? Bali hawa ni watu waasi.
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ فَمَا أَنتَ بِمَلُومٍ
54.
Basi waachilie mbali, nawe hulaumiwi.
وَذَكِّرْ فَإِنَّ الذِّكْرَىٰ تَنفَعُ الْمُؤْمِنِينَ
55.
Na kumbusha, kwani ukumbusho huwafaa Waumini.
وَمَا خَلَقْتُ الْجِنَّ وَالْإِنسَ إِلَّا لِيَعْبُدُونِ
56.
Nami sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi.
مَا أُرِيدُ مِنْهُم مِّن رِّزْقٍ وَمَا أُرِيدُ أَن يُطْعِمُونِ
57.
Na sitaki kwao riziki, wala sitaki wanilishe.
إِنَّ اللَّهَ هُوَ الرَّزَّاقُ ذُو الْقُوَّةِ الْمَتِينُ
58.
Hakika Mwenyezi Mungu ndiye Mwenye kuruzuku, Mwenye nguvu, Madhubuti.
فَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُوا ذَنُوبًا مِّثْلَ ذَنُوبِ أَصْحَابِهِمْ فَلَا يَسْتَعْجِلُونِ
59.
Hakika walio dhulumu wana fungu lao la adhabu kama fungu la wenzao. Basi wasinihimize.
فَوَيْلٌ لِّلَّذِينَ كَفَرُوا مِن يَوْمِهِمُ الَّذِي يُوعَدُونَ
60.
Ole wao walio ikanusha siku yao waliyo ahidiwa.

Maelezo
Imeshuka: Makka
Ina aya: 60
Orodha ya Sura

1. AL-FATIHA
2. AL-BAQARAH
3. AL-'IMRAN
4. AL-NISA'
5. AL-MA'IDAH
6. AL-AN'AM
7. AL-A'RAF
8. AL-ANFAL
9. AL-TAWBAH
10. YUNUS
11. HUD
12. YUSUF
13. AL-RA'D
14. IBRAHIM
15. AL-HIJR
16. AL-NAHL
17. AL-ISRA
18. AL-KAHF
19. MARYAM
20. TAHA
21. AL-ANBIYA'
22. AL-HAJJ
23. AL-MU'MINUNE
24. AL-NUR
25. AL-FURQAN
26. AL-SHU'ARA
27. AL-NAML
28. AL-QASAS
29. AL-'ANKABUT
30. AL-RUM
31. LUQMAN
32. AL-SAJDAH
33. AL-AHZAB
34. SABA'
35. FATIR
36. YASIN
37. AS-SAFFAT
38. SAD
39. Al-ZUMAR
40. GHAFIR
41. FUSSILAT
42. AL-SHURA
43. AL-ZUKHRUF
44. AL-DUKHAN
45. AL-JATHIYAH
46. AL-AHQAF
47. MUHAMMAD
48. AL-FATH
49. AL-HUJURAT
50. QAF
51. AL-DARIYAT
52. AL-TUR
53. AL-NAJM
54. AL-QAMAR
55. AL-RAHMAN
56. AL-WAQI'AH
57. AL-HADID
58. AL-MUJADILAH
59. AL-HASHR
60. AL-MUMTAHANAH
61. AL-SAFF
62. AL-JUMU'AH
63. AL-MUNAFIQUN
64. AL-TAGHABUN
65. AT-TALAQ
66. AT-TAHRIM
67. AL-MULK
68. AL-QALAM
69. AL-HAQQAH
70. AL-MA'ARIJ
71. NUH
72. AL-JINN
73. AL-MUZZAMMIL
74. AL-MUDDATHTHIR
75. AL-QIYAMAH
76. AL-INSAN
77. AL-MURSALATE
78. AN-NABA'
79. AN-NAZI'AT
80. ABASA
81. AL-TAKWIR
82. AL-INFITAR
83. AL-MUTAFFIFIN
84. AL-INSHIQAQ
85. AL-BURUJ
86. AT-TARIQ
87. AL-A'LA
88. AL-GASHIYAH
89. AL-FAJR
90. AL-BALAD
91. AL-SHAMS
92. AL-LAYL
93. AL-DUHA
94. AL-SHARH
95. AT-TIN
96. AL-ALAQ
97. AL-QADR
98. AL-BAYYINAH
99. AL-ZALZALAH
100. AL-'ADIYAT
101. AL-QARI'AH
102. AT-TAKATHUR
103. AL-'ASR
104. AL-HUMAZAH
105. AL-FIL
106. QURAYSH
107. AL-MA'UN
108. AL-KAWTHAR
109. AL-KAFIRUN
110. AL-NASR
111. AL-MASAD
112. AL-IKHLAS
113. AL-FALAQ
114. AL-NAS