Qurani


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

ن ۚ وَالْقَلَمِ وَمَا يَسْطُرُونَ
1.
Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,
مَا أَنتَ بِنِعْمَةِ رَبِّكَ بِمَجْنُونٍ
2.
Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.
وَإِنَّ لَكَ لَأَجْرًا غَيْرَ مَمْنُونٍ
3.
Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.
وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٍ
4.
Na hakika wewe una tabia tukufu.
فَسَتُبْصِرُ وَيُبْصِرُونَ
5.
Karibu utaona, na wao wataona,
بِأَييِّكُمُ الْمَفْتُونُ
6.
Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.
إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعْلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِ وَهُوَ أَعْلَمُ بِالْمُهْتَدِينَ
7.
Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.
فَلَا تُطِعِ الْمُكَذِّبِينَ
8.
Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.
وَدُّوا لَوْ تُدْهِنُ فَيُدْهِنُونَ
9.
Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.
وَلَا تُطِعْ كُلَّ حَلَّافٍ مَّهِينٍ
10.
Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,
هَمَّازٍ مَّشَّاءٍ بِنَمِيمٍ
11.
Mtapitapi, apitaye akifitini,
مَّنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
12.
Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,
عُتُلٍّ بَعْدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ
13.
Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.
أَن كَانَ ذَا مَالٍ وَبَنِينَ
14.
Ati kwa kuwa ana mali na watoto!
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ
15.
Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!
سَنَسِمُهُ عَلَى الْخُرْطُومِ
16.
Tutamtia kovu juu ya pua yake.
إِنَّا بَلَوْنَاهُمْ كَمَا بَلَوْنَا أَصْحَابَ الْجَنَّةِ إِذْ أَقْسَمُوا لَيَصْرِمُنَّهَا مُصْبِحِينَ
17.
Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.
وَلَا يَسْتَثْنُونَ
18.
Wala hawakusema: Mungu akipenda!
فَطَافَ عَلَيْهَا طَائِفٌ مِّن رَّبِّكَ وَهُمْ نَائِمُونَ
19.
Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!
فَأَصْبَحَتْ كَالصَّرِيمِ
20.
Likawa kama usiku wa giza.
فَتَنَادَوْا مُصْبِحِينَ
21.
Asubuhi wakaitana.
أَنِ اغْدُوا عَلَىٰ حَرْثِكُمْ إِن كُنتُمْ صَارِمِينَ
22.
Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.
فَانطَلَقُوا وَهُمْ يَتَخَافَتُونَ
23.
Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,
أَن لَّا يَدْخُلَنَّهَا الْيَوْمَ عَلَيْكُم مِّسْكِينٌ
24.
Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.
وَغَدَوْا عَلَىٰ حَرْدٍ قَادِرِينَ
25.
Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.
فَلَمَّا رَأَوْهَا قَالُوا إِنَّا لَضَالُّونَ
26.
Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
27.
Bali tumenyimwa!
قَالَ أَوْسَطُهُمْ أَلَمْ أَقُل لَّكُمْ لَوْلَا تُسَبِّحُونَ
28.
Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?
قَالُوا سُبْحَانَ رَبِّنَا إِنَّا كُنَّا ظَالِمِينَ
29.
Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.
فَأَقْبَلَ بَعْضُهُمْ عَلَىٰ بَعْضٍ يَتَلَاوَمُونَ
30.
Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.
قَالُوا يَا وَيْلَنَا إِنَّا كُنَّا طَاغِينَ
31.
Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!
عَسَىٰ رَبُّنَا أَن يُبْدِلَنَا خَيْرًا مِّنْهَا إِنَّا إِلَىٰ رَبِّنَا رَاغِبُونَ
32.
Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.
كَذَٰلِكَ الْعَذَابُ ۖ وَلَعَذَابُ الْآخِرَةِ أَكْبَرُ ۚ لَوْ كَانُوا يَعْلَمُونَ
33.
Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتِ النَّعِيمِ
34.
Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.
أَفَنَجْعَلُ الْمُسْلِمِينَ كَالْمُجْرِمِينَ
35.
Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?
مَا لَكُمْ كَيْفَ تَحْكُمُونَ
36.
Mna nini? Mnahukumu vipi?
أَمْ لَكُمْ كِتَابٌ فِيهِ تَدْرُسُونَ
37.
Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?
إِنَّ لَكُمْ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ
38.
Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?
أَمْ لَكُمْ أَيْمَانٌ عَلَيْنَا بَالِغَةٌ إِلَىٰ يَوْمِ الْقِيَامَةِ ۙ إِنَّ لَكُمْ لَمَا تَحْكُمُونَ
39.
Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?
سَلْهُمْ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ
40.
Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?
أَمْ لَهُمْ شُرَكَاءُ فَلْيَأْتُوا بِشُرَكَائِهِمْ إِن كَانُوا صَادِقِينَ
41.
Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.
يَوْمَ يُكْشَفُ عَن سَاقٍ وَيُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ فَلَا يَسْتَطِيعُونَ
42.
Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,
خَاشِعَةً أَبْصَارُهُمْ تَرْهَقُهُمْ ذِلَّةٌ ۖ وَقَدْ كَانُوا يُدْعَوْنَ إِلَى السُّجُودِ وَهُمْ سَالِمُونَ
43.
Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -
فَذَرْنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا الْحَدِيثِ ۖ سَنَسْتَدْرِجُهُم مِّنْ حَيْثُ لَا يَعْلَمُونَ
44.
Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.
وَأُمْلِي لَهُمْ ۚ إِنَّ كَيْدِي مَتِينٌ
45.
Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.
أَمْ تَسْأَلُهُمْ أَجْرًا فَهُم مِّن مَّغْرَمٍ مُّثْقَلُونَ
46.
Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?
أَمْ عِندَهُمُ الْغَيْبُ فَهُمْ يَكْتُبُونَ
47.
Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?
فَاصْبِرْ لِحُكْمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ الْحُوتِ إِذْ نَادَىٰ وَهُوَ مَكْظُومٌ
48.
Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.
لَّوْلَا أَن تَدَارَكَهُ نِعْمَةٌ مِّن رَّبِّهِ لَنُبِذَ بِالْعَرَاءِ وَهُوَ مَذْمُومٌ
49.
Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.
فَاجْتَبَاهُ رَبُّهُ فَجَعَلَهُ مِنَ الصَّالِحِينَ
50.
Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.
وَإِن يَكَادُ الَّذِينَ كَفَرُوا لَيُزْلِقُونَكَ بِأَبْصَارِهِمْ لَمَّا سَمِعُوا الذِّكْرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُ لَمَجْنُونٌ
51.
Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.
وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكْرٌ لِّلْعَالَمِينَ
52.
Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

Maelezo
Imeshuka: Makka
Ina aya: 52
Orodha ya Sura

1. AL-FATIHA
2. AL-BAQARAH
3. AL-'IMRAN
4. AL-NISA'
5. AL-MA'IDAH
6. AL-AN'AM
7. AL-A'RAF
8. AL-ANFAL
9. AL-TAWBAH
10. YUNUS
11. HUD
12. YUSUF
13. AL-RA'D
14. IBRAHIM
15. AL-HIJR
16. AL-NAHL
17. AL-ISRA
18. AL-KAHF
19. MARYAM
20. TAHA
21. AL-ANBIYA'
22. AL-HAJJ
23. AL-MU'MINUNE
24. AL-NUR
25. AL-FURQAN
26. AL-SHU'ARA
27. AL-NAML
28. AL-QASAS
29. AL-'ANKABUT
30. AL-RUM
31. LUQMAN
32. AL-SAJDAH
33. AL-AHZAB
34. SABA'
35. FATIR
36. YASIN
37. AS-SAFFAT
38. SAD
39. Al-ZUMAR
40. GHAFIR
41. FUSSILAT
42. AL-SHURA
43. AL-ZUKHRUF
44. AL-DUKHAN
45. AL-JATHIYAH
46. AL-AHQAF
47. MUHAMMAD
48. AL-FATH
49. AL-HUJURAT
50. QAF
51. AL-DARIYAT
52. AL-TUR
53. AL-NAJM
54. AL-QAMAR
55. AL-RAHMAN
56. AL-WAQI'AH
57. AL-HADID
58. AL-MUJADILAH
59. AL-HASHR
60. AL-MUMTAHANAH
61. AL-SAFF
62. AL-JUMU'AH
63. AL-MUNAFIQUN
64. AL-TAGHABUN
65. AT-TALAQ
66. AT-TAHRIM
67. AL-MULK
68. AL-QALAM
69. AL-HAQQAH
70. AL-MA'ARIJ
71. NUH
72. AL-JINN
73. AL-MUZZAMMIL
74. AL-MUDDATHTHIR
75. AL-QIYAMAH
76. AL-INSAN
77. AL-MURSALATE
78. AN-NABA'
79. AN-NAZI'AT
80. ABASA
81. AL-TAKWIR
82. AL-INFITAR
83. AL-MUTAFFIFIN
84. AL-INSHIQAQ
85. AL-BURUJ
86. AT-TARIQ
87. AL-A'LA
88. AL-GASHIYAH
89. AL-FAJR
90. AL-BALAD
91. AL-SHAMS
92. AL-LAYL
93. AL-DUHA
94. AL-SHARH
95. AT-TIN
96. AL-ALAQ
97. AL-QADR
98. AL-BAYYINAH
99. AL-ZALZALAH
100. AL-'ADIYAT
101. AL-QARI'AH
102. AT-TAKATHUR
103. AL-'ASR
104. AL-HUMAZAH
105. AL-FIL
106. QURAYSH
107. AL-MA'UN
108. AL-KAWTHAR
109. AL-KAFIRUN
110. AL-NASR
111. AL-MASAD
112. AL-IKHLAS
113. AL-FALAQ
114. AL-NAS