Qurani


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

إِذَا وَقَعَتِ الْوَاقِعَةُ
1.
Litakapo tukia hilo Tukio
لَيْسَ لِوَقْعَتِهَا كَاذِبَةٌ
2.
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
خَافِضَةٌ رَّافِعَةٌ
3.
Literemshalo linyanyualo,
إِذَا رُجَّتِ الْأَرْضُ رَجًّا
4.
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
وَبُسَّتِ الْجِبَالُ بَسًّا
5.
Na milima itapo sagwasagwa,
فَكَانَتْ هَبَاءً مُّنبَثًّا
6.
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
وَكُنتُمْ أَزْوَاجًا ثَلَاثَةً
7.
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
فَأَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَيْمَنَةِ
8.
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
وَأَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ مَا أَصْحَابُ الْمَشْأَمَةِ
9.
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ
10.
Na wa mbele watakuwa mbele.
أُولَٰئِكَ الْمُقَرَّبُونَ
11.
Hao ndio watakao karibishwa
فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ
12.
Katika Bustani zenye neema.
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ
13.
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ
14.
Na wachache katika wa mwisho.
عَلَىٰ سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ
15.
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
مُّتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ
16.
Wakiviegemea wakielekeana.
يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ
17.
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ
18.
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ
19.
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ
20.
Na matunda wayapendayo,
وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ
21.
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
وَحُورٌ عِينٌ
22.
Na Mahurulaini,
كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ
23.
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
جَزَاءً بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ
24.
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا
25.
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا
26.
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ
27.
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ
28.
Katika mikunazi isiyo na miba,
وَطَلْحٍ مَّنضُودٍ
29.
Na migomba iliyo pangiliwa,
وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ
30.
Na kivuli kilicho tanda,
وَمَاءٍ مَّسْكُوبٍ
31.
Na maji yanayo miminika,
وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ
32.
Na matunda mengi,
لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ
33.
Hayatindikii wala hayakatazwi,
وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ
34.
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاءً
35.
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًا
36.
Na tutawafanya vijana,
عُرُبًا أَتْرَابًا
37.
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ
38.
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ
39.
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ
40.
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
وَأَصْحَابُ الشِّمَالِ مَا أَصْحَابُ الشِّمَالِ
41.
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
فِي سَمُومٍ وَحَمِيمٍ
42.
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
وَظِلٍّ مِّن يَحْمُومٍ
43.
Na kivuli cha moshi mweusi,
لَّا بَارِدٍ وَلَا كَرِيمٍ
44.
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَٰلِكَ مُتْرَفِينَ
45.
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
وَكَانُوا يُصِرُّونَ عَلَى الْحِنثِ الْعَظِيمِ
46.
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
وَكَانُوا يَقُولُونَ أَئِذَا مِتْنَا وَكُنَّا تُرَابًا وَعِظَامًا أَإِنَّا لَمَبْعُوثُونَ
47.
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
أَوَآبَاؤُنَا الْأَوَّلُونَ
48.
Au baba zetu wa zamani?
قُلْ إِنَّ الْأَوَّلِينَ وَالْآخِرِينَ
49.
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
لَمَجْمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَاتِ يَوْمٍ مَّعْلُومٍ
50.
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
ثُمَّ إِنَّكُمْ أَيُّهَا الضَّالُّونَ الْمُكَذِّبُونَ
51.
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
لَآكِلُونَ مِن شَجَرٍ مِّن زَقُّومٍ
52.
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
فَمَالِئُونَ مِنْهَا الْبُطُونَ
53.
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
فَشَارِبُونَ عَلَيْهِ مِنَ الْحَمِيمِ
54.
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
فَشَارِبُونَ شُرْبَ الْهِيمِ
55.
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
هَٰذَا نُزُلُهُمْ يَوْمَ الدِّينِ
56.
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
نَحْنُ خَلَقْنَاكُمْ فَلَوْلَا تُصَدِّقُونَ
57.
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
أَفَرَأَيْتُم مَّا تُمْنُونَ
58.
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
أَأَنتُمْ تَخْلُقُونَهُ أَمْ نَحْنُ الْخَالِقُونَ
59.
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
نَحْنُ قَدَّرْنَا بَيْنَكُمُ الْمَوْتَ وَمَا نَحْنُ بِمَسْبُوقِينَ
60.
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
عَلَىٰ أَن نُّبَدِّلَ أَمْثَالَكُمْ وَنُنشِئَكُمْ فِي مَا لَا تَعْلَمُونَ
61.
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
وَلَقَدْ عَلِمْتُمُ النَّشْأَةَ الْأُولَىٰ فَلَوْلَا تَذَكَّرُونَ
62.
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
أَفَرَأَيْتُم مَّا تَحْرُثُونَ
63.
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
أَأَنتُمْ تَزْرَعُونَهُ أَمْ نَحْنُ الزَّارِعُونَ
64.
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
لَوْ نَشَاءُ لَجَعَلْنَاهُ حُطَامًا فَظَلْتُمْ تَفَكَّهُونَ
65.
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
إِنَّا لَمُغْرَمُونَ
66.
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
بَلْ نَحْنُ مَحْرُومُونَ
67.
Bali sisi tumenyimwa.
أَفَرَأَيْتُمُ الْمَاءَ الَّذِي تَشْرَبُونَ
68.
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
أَأَنتُمْ أَنزَلْتُمُوهُ مِنَ الْمُزْنِ أَمْ نَحْنُ الْمُنزِلُونَ
69.
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
لَوْ نَشَاءُ جَعَلْنَاهُ أُجَاجًا فَلَوْلَا تَشْكُرُونَ
70.
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
أَفَرَأَيْتُمُ النَّارَ الَّتِي تُورُونَ
71.
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
أَأَنتُمْ أَنشَأْتُمْ شَجَرَتَهَا أَمْ نَحْنُ الْمُنشِئُونَ
72.
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
نَحْنُ جَعَلْنَاهَا تَذْكِرَةً وَمَتَاعًا لِّلْمُقْوِينَ
73.
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ
74.
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
فَلَا أُقْسِمُ بِمَوَاقِعِ النُّجُومِ
75.
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
وَإِنَّهُ لَقَسَمٌ لَّوْ تَعْلَمُونَ عَظِيمٌ
76.
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
إِنَّهُ لَقُرْآنٌ كَرِيمٌ
77.
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
فِي كِتَابٍ مَّكْنُونٍ
78.
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
لَّا يَمَسُّهُ إِلَّا الْمُطَهَّرُونَ
79.
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
تَنزِيلٌ مِّن رَّبِّ الْعَالَمِينَ
80.
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَفَبِهَٰذَا الْحَدِيثِ أَنتُم مُّدْهِنُونَ
81.
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
وَتَجْعَلُونَ رِزْقَكُمْ أَنَّكُمْ تُكَذِّبُونَ
82.
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
فَلَوْلَا إِذَا بَلَغَتِ الْحُلْقُومَ
83.
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
وَأَنتُمْ حِينَئِذٍ تَنظُرُونَ
84.
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
وَنَحْنُ أَقْرَبُ إِلَيْهِ مِنكُمْ وَلَٰكِن لَّا تُبْصِرُونَ
85.
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
فَلَوْلَا إِن كُنتُمْ غَيْرَ مَدِينِينَ
86.
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
تَرْجِعُونَهَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ
87.
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
فَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُقَرَّبِينَ
88.
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
فَرَوْحٌ وَرَيْحَانٌ وَجَنَّتُ نَعِيمٍ
89.
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ
90.
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
فَسَلَامٌ لَّكَ مِنْ أَصْحَابِ الْيَمِينِ
91.
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
وَأَمَّا إِن كَانَ مِنَ الْمُكَذِّبِينَ الضَّالِّينَ
92.
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
فَنُزُلٌ مِّنْ حَمِيمٍ
93.
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
وَتَصْلِيَةُ جَحِيمٍ
94.
Na kutiwa Motoni.
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ الْيَقِينِ
95.
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
فَسَبِّحْ بِاسْمِ رَبِّكَ الْعَظِيمِ
96.
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.

Maelezo
Imeshuka: Makka
Ina aya: 96
Orodha ya Sura

1. AL-FATIHA
2. AL-BAQARAH
3. AL-'IMRAN
4. AL-NISA'
5. AL-MA'IDAH
6. AL-AN'AM
7. AL-A'RAF
8. AL-ANFAL
9. AL-TAWBAH
10. YUNUS
11. HUD
12. YUSUF
13. AL-RA'D
14. IBRAHIM
15. AL-HIJR
16. AL-NAHL
17. AL-ISRA
18. AL-KAHF
19. MARYAM
20. TAHA
21. AL-ANBIYA'
22. AL-HAJJ
23. AL-MU'MINUNE
24. AL-NUR
25. AL-FURQAN
26. AL-SHU'ARA
27. AL-NAML
28. AL-QASAS
29. AL-'ANKABUT
30. AL-RUM
31. LUQMAN
32. AL-SAJDAH
33. AL-AHZAB
34. SABA'
35. FATIR
36. YASIN
37. AS-SAFFAT
38. SAD
39. Al-ZUMAR
40. GHAFIR
41. FUSSILAT
42. AL-SHURA
43. AL-ZUKHRUF
44. AL-DUKHAN
45. AL-JATHIYAH
46. AL-AHQAF
47. MUHAMMAD
48. AL-FATH
49. AL-HUJURAT
50. QAF
51. AL-DARIYAT
52. AL-TUR
53. AL-NAJM
54. AL-QAMAR
55. AL-RAHMAN
56. AL-WAQI'AH
57. AL-HADID
58. AL-MUJADILAH
59. AL-HASHR
60. AL-MUMTAHANAH
61. AL-SAFF
62. AL-JUMU'AH
63. AL-MUNAFIQUN
64. AL-TAGHABUN
65. AT-TALAQ
66. AT-TAHRIM
67. AL-MULK
68. AL-QALAM
69. AL-HAQQAH
70. AL-MA'ARIJ
71. NUH
72. AL-JINN
73. AL-MUZZAMMIL
74. AL-MUDDATHTHIR
75. AL-QIYAMAH
76. AL-INSAN
77. AL-MURSALATE
78. AN-NABA'
79. AN-NAZI'AT
80. ABASA
81. AL-TAKWIR
82. AL-INFITAR
83. AL-MUTAFFIFIN
84. AL-INSHIQAQ
85. AL-BURUJ
86. AT-TARIQ
87. AL-A'LA
88. AL-GASHIYAH
89. AL-FAJR
90. AL-BALAD
91. AL-SHAMS
92. AL-LAYL
93. AL-DUHA
94. AL-SHARH
95. AT-TIN
96. AL-ALAQ
97. AL-QADR
98. AL-BAYYINAH
99. AL-ZALZALAH
100. AL-'ADIYAT
101. AL-QARI'AH
102. AT-TAKATHUR
103. AL-'ASR
104. AL-HUMAZAH
105. AL-FIL
106. QURAYSH
107. AL-MA'UN
108. AL-KAWTHAR
109. AL-KAFIRUN
110. AL-NASR
111. AL-MASAD
112. AL-IKHLAS
113. AL-FALAQ
114. AL-NAS