Qurani


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

وَالنَّازِعَاتِ غَرْقًا
1.
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
وَالنَّاشِطَاتِ نَشْطًا
2.
Na kwa wanao toa kwa upole,
وَالسَّابِحَاتِ سَبْحًا
3.
Na wanao ogelea,
فَالسَّابِقَاتِ سَبْقًا
4.
Wakishindana mbio,
فَالْمُدَبِّرَاتِ أَمْرًا
5.
Wakidabiri mambo.
يَوْمَ تَرْجُفُ الرَّاجِفَةُ
6.
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
تَتْبَعُهَا الرَّادِفَةُ
7.
Kifuate cha kufuatia.
قُلُوبٌ يَوْمَئِذٍ وَاجِفَةٌ
8.
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
أَبْصَارُهَا خَاشِعَةٌ
9.
Macho yatainama chini.
يَقُولُونَ أَإِنَّا لَمَرْدُودُونَ فِي الْحَافِرَةِ
10.
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
أَإِذَا كُنَّا عِظَامًا نَّخِرَةً
11.
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
قَالُوا تِلْكَ إِذًا كَرَّةٌ خَاسِرَةٌ
12.
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
فَإِنَّمَا هِيَ زَجْرَةٌ وَاحِدَةٌ
13.
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
فَإِذَا هُم بِالسَّاهِرَةِ
14.
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ مُوسَىٰ
15.
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
إِذْ نَادَاهُ رَبُّهُ بِالْوَادِ الْمُقَدَّسِ طُوًى
16.
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
اذْهَبْ إِلَىٰ فِرْعَوْنَ إِنَّهُ طَغَىٰ
17.
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
فَقُلْ هَل لَّكَ إِلَىٰ أَن تَزَكَّىٰ
18.
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
وَأَهْدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخْشَىٰ
19.
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
فَأَرَاهُ الْآيَةَ الْكُبْرَىٰ
20.
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ
21.
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
ثُمَّ أَدْبَرَ يَسْعَىٰ
22.
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ
23.
Akakusanya watu akanadi.
فَقَالَ أَنَا رَبُّكُمُ الْأَعْلَىٰ
24.
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
فَأَخَذَهُ اللَّهُ نَكَالَ الْآخِرَةِ وَالْأُولَىٰ
25.
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبْرَةً لِّمَن يَخْشَىٰ
26.
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
أَأَنتُمْ أَشَدُّ خَلْقًا أَمِ السَّمَاءُ ۚ بَنَاهَا
27.
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
رَفَعَ سَمْكَهَا فَسَوَّاهَا
28.
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
وَأَغْطَشَ لَيْلَهَا وَأَخْرَجَ ضُحَاهَا
29.
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
وَالْأَرْضَ بَعْدَ ذَٰلِكَ دَحَاهَا
30.
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
أَخْرَجَ مِنْهَا مَاءَهَا وَمَرْعَاهَا
31.
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
وَالْجِبَالَ أَرْسَاهَا
32.
Na milima akaisimamisha,
مَتَاعًا لَّكُمْ وَلِأَنْعَامِكُمْ
33.
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَاءَتِ الطَّامَّةُ الْكُبْرَىٰ
34.
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
يَوْمَ يَتَذَكَّرُ الْإِنسَانُ مَا سَعَىٰ
35.
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
وَبُرِّزَتِ الْجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ
36.
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ
37.
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
وَآثَرَ الْحَيَاةَ الدُّنْيَا
38.
Na akakhiari maisha ya dunia,
فَإِنَّ الْجَحِيمَ هِيَ الْمَأْوَىٰ
39.
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
وَأَمَّا مَنْ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِ وَنَهَى النَّفْسَ عَنِ الْهَوَىٰ
40.
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
فَإِنَّ الْجَنَّةَ هِيَ الْمَأْوَىٰ
41.
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
يَسْأَلُونَكَ عَنِ السَّاعَةِ أَيَّانَ مُرْسَاهَا
42.
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكْرَاهَا
43.
Una nini wewe hata uitaje?
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَاهَا
44.
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
إِنَّمَا أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخْشَاهَا
45.
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
كَأَنَّهُمْ يَوْمَ يَرَوْنَهَا لَمْ يَلْبَثُوا إِلَّا عَشِيَّةً أَوْ ضُحَاهَا
46.
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.

Maelezo
Imeshuka: Makka
Ina aya: 46
Orodha ya Sura

1. AL-FATIHA
2. AL-BAQARAH
3. AL-'IMRAN
4. AL-NISA'
5. AL-MA'IDAH
6. AL-AN'AM
7. AL-A'RAF
8. AL-ANFAL
9. AL-TAWBAH
10. YUNUS
11. HUD
12. YUSUF
13. AL-RA'D
14. IBRAHIM
15. AL-HIJR
16. AL-NAHL
17. AL-ISRA
18. AL-KAHF
19. MARYAM
20. TAHA
21. AL-ANBIYA'
22. AL-HAJJ
23. AL-MU'MINUNE
24. AL-NUR
25. AL-FURQAN
26. AL-SHU'ARA
27. AL-NAML
28. AL-QASAS
29. AL-'ANKABUT
30. AL-RUM
31. LUQMAN
32. AL-SAJDAH
33. AL-AHZAB
34. SABA'
35. FATIR
36. YASIN
37. AS-SAFFAT
38. SAD
39. Al-ZUMAR
40. GHAFIR
41. FUSSILAT
42. AL-SHURA
43. AL-ZUKHRUF
44. AL-DUKHAN
45. AL-JATHIYAH
46. AL-AHQAF
47. MUHAMMAD
48. AL-FATH
49. AL-HUJURAT
50. QAF
51. AL-DARIYAT
52. AL-TUR
53. AL-NAJM
54. AL-QAMAR
55. AL-RAHMAN
56. AL-WAQI'AH
57. AL-HADID
58. AL-MUJADILAH
59. AL-HASHR
60. AL-MUMTAHANAH
61. AL-SAFF
62. AL-JUMU'AH
63. AL-MUNAFIQUN
64. AL-TAGHABUN
65. AT-TALAQ
66. AT-TAHRIM
67. AL-MULK
68. AL-QALAM
69. AL-HAQQAH
70. AL-MA'ARIJ
71. NUH
72. AL-JINN
73. AL-MUZZAMMIL
74. AL-MUDDATHTHIR
75. AL-QIYAMAH
76. AL-INSAN
77. AL-MURSALATE
78. AN-NABA'
79. AN-NAZI'AT
80. ABASA
81. AL-TAKWIR
82. AL-INFITAR
83. AL-MUTAFFIFIN
84. AL-INSHIQAQ
85. AL-BURUJ
86. AT-TARIQ
87. AL-A'LA
88. AL-GASHIYAH
89. AL-FAJR
90. AL-BALAD
91. AL-SHAMS
92. AL-LAYL
93. AL-DUHA
94. AL-SHARH
95. AT-TIN
96. AL-ALAQ
97. AL-QADR
98. AL-BAYYINAH
99. AL-ZALZALAH
100. AL-'ADIYAT
101. AL-QARI'AH
102. AT-TAKATHUR
103. AL-'ASR
104. AL-HUMAZAH
105. AL-FIL
106. QURAYSH
107. AL-MA'UN
108. AL-KAWTHAR
109. AL-KAFIRUN
110. AL-NASR
111. AL-MASAD
112. AL-IKHLAS
113. AL-FALAQ
114. AL-NAS