Qurani


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

لَا أُقْسِمُ بِيَوْمِ الْقِيَامَةِ
1.
Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!
وَلَا أُقْسِمُ بِالنَّفْسِ اللَّوَّامَةِ
2.
Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَلَّن نَّجْمَعَ عِظَامَهُ
3.
Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
بَلَىٰ قَادِرِينَ عَلَىٰ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُ
4.
Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!
بَلْ يُرِيدُ الْإِنسَانُ لِيَفْجُرَ أَمَامَهُ
5.
Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.
يَسْأَلُ أَيَّانَ يَوْمُ الْقِيَامَةِ
6.
Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?
فَإِذَا بَرِقَ الْبَصَرُ
7.
Basi jicho litapo dawaa,
وَخَسَفَ الْقَمَرُ
8.
Na mwezi utapo patwa,
وَجُمِعَ الشَّمْسُ وَالْقَمَرُ
9.
Na likakusanywa jua na mwezi,
يَقُولُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ أَيْنَ الْمَفَرُّ
10.
Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?
كَلَّا لَا وَزَرَ
11.
La! Hapana pa kukimbilia!
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمُسْتَقَرُّ
12.
Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.
يُنَبَّأُ الْإِنسَانُ يَوْمَئِذٍ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
13.
Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.
بَلِ الْإِنسَانُ عَلَىٰ نَفْسِهِ بَصِيرَةٌ
14.
Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.
وَلَوْ أَلْقَىٰ مَعَاذِيرَهُ
15.
Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.
لَا تُحَرِّكْ بِهِ لِسَانَكَ لِتَعْجَلَ بِهِ
16.
Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.
إِنَّ عَلَيْنَا جَمْعَهُ وَقُرْآنَهُ
17.
Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.
فَإِذَا قَرَأْنَاهُ فَاتَّبِعْ قُرْآنَهُ
18.
Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيْنَا بَيَانَهُ
19.
Kisha ni juu yetu kuubainisha.
كَلَّا بَلْ تُحِبُّونَ الْعَاجِلَةَ
20.
Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,
وَتَذَرُونَ الْآخِرَةَ
21.
Na mnaacha maisha ya Akhera.
وُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ نَّاضِرَةٌ
22.
Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,
إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٌ
23.
Zinamwangallia Mola wao Mlezi.
وَوُجُوهٌ يَوْمَئِذٍ بَاسِرَةٌ
24.
Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.
تَظُنُّ أَن يُفْعَلَ بِهَا فَاقِرَةٌ
25.
Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.
كَلَّا إِذَا بَلَغَتِ التَّرَاقِيَ
26.
La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,
وَقِيلَ مَنْ ۜ رَاقٍ
27.
Na pakasemwa: Nani wa kumganga?
وَظَنَّ أَنَّهُ الْفِرَاقُ
28.
Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;
وَالْتَفَّتِ السَّاقُ بِالسَّاقِ
29.
Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوْمَئِذٍ الْمَسَاقُ
30.
Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!
فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ
31.
Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.
وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ
32.
Bali alikanusha, na akageuka.
ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰ أَهْلِهِ يَتَمَطَّىٰ
33.
Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.
أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ
34.
Ole wako, ole wako!
ثُمَّ أَوْلَىٰ لَكَ فَأَوْلَىٰ
35.
Kisha Ole wako, ole wako!
أَيَحْسَبُ الْإِنسَانُ أَن يُتْرَكَ سُدًى
36.
Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?
أَلَمْ يَكُ نُطْفَةً مِّن مَّنِيٍّ يُمْنَىٰ
37.
Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?
ثُمَّ كَانَ عَلَقَةً فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ
38.
Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.
فَجَعَلَ مِنْهُ الزَّوْجَيْنِ الذَّكَرَ وَالْأُنثَىٰ
39.
Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.
أَلَيْسَ ذَٰلِكَ بِقَادِرٍ عَلَىٰ أَن يُحْيِيَ الْمَوْتَىٰ
40.
Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?

Maelezo
Imeshuka: Makka
Ina aya: 40
Orodha ya Sura

1. AL-FATIHA
2. AL-BAQARAH
3. AL-'IMRAN
4. AL-NISA'
5. AL-MA'IDAH
6. AL-AN'AM
7. AL-A'RAF
8. AL-ANFAL
9. AL-TAWBAH
10. YUNUS
11. HUD
12. YUSUF
13. AL-RA'D
14. IBRAHIM
15. AL-HIJR
16. AL-NAHL
17. AL-ISRA
18. AL-KAHF
19. MARYAM
20. TAHA
21. AL-ANBIYA'
22. AL-HAJJ
23. AL-MU'MINUNE
24. AL-NUR
25. AL-FURQAN
26. AL-SHU'ARA
27. AL-NAML
28. AL-QASAS
29. AL-'ANKABUT
30. AL-RUM
31. LUQMAN
32. AL-SAJDAH
33. AL-AHZAB
34. SABA'
35. FATIR
36. YASIN
37. AS-SAFFAT
38. SAD
39. Al-ZUMAR
40. GHAFIR
41. FUSSILAT
42. AL-SHURA
43. AL-ZUKHRUF
44. AL-DUKHAN
45. AL-JATHIYAH
46. AL-AHQAF
47. MUHAMMAD
48. AL-FATH
49. AL-HUJURAT
50. QAF
51. AL-DARIYAT
52. AL-TUR
53. AL-NAJM
54. AL-QAMAR
55. AL-RAHMAN
56. AL-WAQI'AH
57. AL-HADID
58. AL-MUJADILAH
59. AL-HASHR
60. AL-MUMTAHANAH
61. AL-SAFF
62. AL-JUMU'AH
63. AL-MUNAFIQUN
64. AL-TAGHABUN
65. AT-TALAQ
66. AT-TAHRIM
67. AL-MULK
68. AL-QALAM
69. AL-HAQQAH
70. AL-MA'ARIJ
71. NUH
72. AL-JINN
73. AL-MUZZAMMIL
74. AL-MUDDATHTHIR
75. AL-QIYAMAH
76. AL-INSAN
77. AL-MURSALATE
78. AN-NABA'
79. AN-NAZI'AT
80. ABASA
81. AL-TAKWIR
82. AL-INFITAR
83. AL-MUTAFFIFIN
84. AL-INSHIQAQ
85. AL-BURUJ
86. AT-TARIQ
87. AL-A'LA
88. AL-GASHIYAH
89. AL-FAJR
90. AL-BALAD
91. AL-SHAMS
92. AL-LAYL
93. AL-DUHA
94. AL-SHARH
95. AT-TIN
96. AL-ALAQ
97. AL-QADR
98. AL-BAYYINAH
99. AL-ZALZALAH
100. AL-'ADIYAT
101. AL-QARI'AH
102. AT-TAKATHUR
103. AL-'ASR
104. AL-HUMAZAH
105. AL-FIL
106. QURAYSH
107. AL-MA'UN
108. AL-KAWTHAR
109. AL-KAFIRUN
110. AL-NASR
111. AL-MASAD
112. AL-IKHLAS
113. AL-FALAQ
114. AL-NAS