Qurani


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

عَمَّ يَتَسَاءَلُونَ
1.
WANAULIZANA nini?
عَنِ النَّبَإِ الْعَظِيمِ
2.
Ile khabari kuu,
الَّذِي هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ
3.
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
4.
La! Karibu watakuja jua.
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ
5.
Tena la! Karibu watakuja jua.
أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ مِهَادًا
6.
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
وَالْجِبَالَ أَوْتَادًا
7.
Na milima kama vigingi?
وَخَلَقْنَاكُمْ أَزْوَاجًا
8.
Na tukakuumbeni kwa jozi?
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًا
9.
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
وَجَعَلْنَا اللَّيْلَ لِبَاسًا
10.
Na tukaufanya usiku ni nguo?
وَجَعَلْنَا النَّهَارَ مَعَاشًا
11.
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًا شِدَادًا
12.
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
وَجَعَلْنَا سِرَاجًا وَهَّاجًا
13.
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
وَأَنزَلْنَا مِنَ الْمُعْصِرَاتِ مَاءً ثَجَّاجًا
14.
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
لِّنُخْرِجَ بِهِ حَبًّا وَنَبَاتًا
15.
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
وَجَنَّاتٍ أَلْفَافًا
16.
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ كَانَ مِيقَاتًا
17.
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًا
18.
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
وَفُتِحَتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ أَبْوَابًا
19.
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
وَسُيِّرَتِ الْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا
20.
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا
21.
Hakika Jahannamu inangojea!
لِّلطَّاغِينَ مَآبًا
22.
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
لَّابِثِينَ فِيهَا أَحْقَابًا
23.
Wakae humo karne baada ya karne,
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا
24.
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا
25.
Ila maji yamoto sana na usaha,
جَزَاءً وِفَاقًا
26.
Ndio jaza muwafaka.
إِنَّهُمْ كَانُوا لَا يَرْجُونَ حِسَابًا
27.
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كِذَّابًا
28.
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ كِتَابًا
29.
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
فَذُوقُوا فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا
30.
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا
31.
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا
32.
Mabustani na mizabibu,
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا
33.
Na wake walio lingana nao,
وَكَأْسًا دِهَاقًا
34.
Na bilauri zilizo jaa,
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا
35.
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
جَزَاءً مِّن رَّبِّكَ عَطَاءً حِسَابًا
36.
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
رَّبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الرَّحْمَٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًا
37.
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَٰنُ وَقَالَ صَوَابًا
38.
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الْحَقُّ ۖ فَمَن شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ مَآبًا
39.
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
إِنَّا أَنذَرْنَاكُمْ عَذَابًا قَرِيبًا يَوْمَ يَنظُرُ الْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ الْكَافِرُ يَا لَيْتَنِي كُنتُ تُرَابًا
40.
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!

Maelezo
Imeshuka: Makka
Ina aya: 40
Orodha ya Sura

1. AL-FATIHA
2. AL-BAQARAH
3. AL-'IMRAN
4. AL-NISA'
5. AL-MA'IDAH
6. AL-AN'AM
7. AL-A'RAF
8. AL-ANFAL
9. AL-TAWBAH
10. YUNUS
11. HUD
12. YUSUF
13. AL-RA'D
14. IBRAHIM
15. AL-HIJR
16. AL-NAHL
17. AL-ISRA
18. AL-KAHF
19. MARYAM
20. TAHA
21. AL-ANBIYA'
22. AL-HAJJ
23. AL-MU'MINUNE
24. AL-NUR
25. AL-FURQAN
26. AL-SHU'ARA
27. AL-NAML
28. AL-QASAS
29. AL-'ANKABUT
30. AL-RUM
31. LUQMAN
32. AL-SAJDAH
33. AL-AHZAB
34. SABA'
35. FATIR
36. YASIN
37. AS-SAFFAT
38. SAD
39. Al-ZUMAR
40. GHAFIR
41. FUSSILAT
42. AL-SHURA
43. AL-ZUKHRUF
44. AL-DUKHAN
45. AL-JATHIYAH
46. AL-AHQAF
47. MUHAMMAD
48. AL-FATH
49. AL-HUJURAT
50. QAF
51. AL-DARIYAT
52. AL-TUR
53. AL-NAJM
54. AL-QAMAR
55. AL-RAHMAN
56. AL-WAQI'AH
57. AL-HADID
58. AL-MUJADILAH
59. AL-HASHR
60. AL-MUMTAHANAH
61. AL-SAFF
62. AL-JUMU'AH
63. AL-MUNAFIQUN
64. AL-TAGHABUN
65. AT-TALAQ
66. AT-TAHRIM
67. AL-MULK
68. AL-QALAM
69. AL-HAQQAH
70. AL-MA'ARIJ
71. NUH
72. AL-JINN
73. AL-MUZZAMMIL
74. AL-MUDDATHTHIR
75. AL-QIYAMAH
76. AL-INSAN
77. AL-MURSALATE
78. AN-NABA'
79. AN-NAZI'AT
80. ABASA
81. AL-TAKWIR
82. AL-INFITAR
83. AL-MUTAFFIFIN
84. AL-INSHIQAQ
85. AL-BURUJ
86. AT-TARIQ
87. AL-A'LA
88. AL-GASHIYAH
89. AL-FAJR
90. AL-BALAD
91. AL-SHAMS
92. AL-LAYL
93. AL-DUHA
94. AL-SHARH
95. AT-TIN
96. AL-ALAQ
97. AL-QADR
98. AL-BAYYINAH
99. AL-ZALZALAH
100. AL-'ADIYAT
101. AL-QARI'AH
102. AT-TAKATHUR
103. AL-'ASR
104. AL-HUMAZAH
105. AL-FIL
106. QURAYSH
107. AL-MA'UN
108. AL-KAWTHAR
109. AL-KAFIRUN
110. AL-NASR
111. AL-MASAD
112. AL-IKHLAS
113. AL-FALAQ
114. AL-NAS