Qurani


KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU

وَيْلٌ لِّلْمُطَفِّفِينَ
1.
Ole wao hao wapunjao!
الَّذِينَ إِذَا اكْتَالُوا عَلَى النَّاسِ يَسْتَوْفُونَ
2.
Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.
وَإِذَا كَالُوهُمْ أَو وَّزَنُوهُمْ يُخْسِرُونَ
3.
Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.
أَلَا يَظُنُّ أُولَٰئِكَ أَنَّهُم مَّبْعُوثُونَ
4.
Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa
لِيَوْمٍ عَظِيمٍ
5.
Katika Siku iliyo kuu,
يَوْمَ يَقُومُ النَّاسُ لِرَبِّ الْعَالَمِينَ
6.
Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٍ
7.
Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا سِجِّينٌ
8.
Unajua nini Sijjin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ
9.
Kitabu kilicho andikwa.
وَيْلٌ يَوْمَئِذٍ لِّلْمُكَذِّبِينَ
10.
Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!
الَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوْمِ الدِّينِ
11.
Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.
وَمَا يُكَذِّبُ بِهِ إِلَّا كُلُّ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ
12.
Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.
إِذَا تُتْلَىٰ عَلَيْهِ آيَاتُنَا قَالَ أَسَاطِيرُ الْأَوَّلِينَ
13.
Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!
كَلَّا ۖ بَلْ ۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُوا يَكْسِبُونَ
14.
Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.
كَلَّا إِنَّهُمْ عَن رَّبِّهِمْ يَوْمَئِذٍ لَّمَحْجُوبُونَ
15.
Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.
ثُمَّ إِنَّهُمْ لَصَالُو الْجَحِيمِ
16.
Kisha wataingia Motoni!
ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا الَّذِي كُنتُم بِهِ تُكَذِّبُونَ
17.
Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.
كَلَّا إِنَّ كِتَابَ الْأَبْرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ
18.
Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.
وَمَا أَدْرَاكَ مَا عِلِّيُّونَ
19.
Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?
كِتَابٌ مَّرْقُومٌ
20.
Kitabu kilicho andikwa.
يَشْهَدُهُ الْمُقَرَّبُونَ
21.
Wanakishuhudia walio karibishwa.
إِنَّ الْأَبْرَارَ لَفِي نَعِيمٍ
22.
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ
23.
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.
تَعْرِفُ فِي وُجُوهِهِمْ نَضْرَةَ النَّعِيمِ
24.
Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,
يُسْقَوْنَ مِن رَّحِيقٍ مَّخْتُومٍ
25.
Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,
خِتَامُهُ مِسْكٌ ۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلْيَتَنَافَسِ الْمُتَنَافِسُونَ
26.
Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.
وَمِزَاجُهُ مِن تَسْنِيمٍ
27.
Na mchanganyiko wake ni Tasniim,
عَيْنًا يَشْرَبُ بِهَا الْمُقَرَّبُونَ
28.
Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.
إِنَّ الَّذِينَ أَجْرَمُوا كَانُوا مِنَ الَّذِينَ آمَنُوا يَضْحَكُونَ
29.
Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.
وَإِذَا مَرُّوا بِهِمْ يَتَغَامَزُونَ
30.
Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.
وَإِذَا انقَلَبُوا إِلَىٰ أَهْلِهِمُ انقَلَبُوا فَكِهِينَ
31.
Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.
وَإِذَا رَأَوْهُمْ قَالُوا إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَضَالُّونَ
32.
Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.
وَمَا أُرْسِلُوا عَلَيْهِمْ حَافِظِينَ
33.
Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.
فَالْيَوْمَ الَّذِينَ آمَنُوا مِنَ الْكُفَّارِ يَضْحَكُونَ
34.
Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,
عَلَى الْأَرَائِكِ يَنظُرُونَ
35.
Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.
هَلْ ثُوِّبَ الْكُفَّارُ مَا كَانُوا يَفْعَلُونَ
36.
Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?

Maelezo
Imeshuka: Makka
Ina aya: 36
Orodha ya Sura

1. AL-FATIHA
2. AL-BAQARAH
3. AL-'IMRAN
4. AL-NISA'
5. AL-MA'IDAH
6. AL-AN'AM
7. AL-A'RAF
8. AL-ANFAL
9. AL-TAWBAH
10. YUNUS
11. HUD
12. YUSUF
13. AL-RA'D
14. IBRAHIM
15. AL-HIJR
16. AL-NAHL
17. AL-ISRA
18. AL-KAHF
19. MARYAM
20. TAHA
21. AL-ANBIYA'
22. AL-HAJJ
23. AL-MU'MINUNE
24. AL-NUR
25. AL-FURQAN
26. AL-SHU'ARA
27. AL-NAML
28. AL-QASAS
29. AL-'ANKABUT
30. AL-RUM
31. LUQMAN
32. AL-SAJDAH
33. AL-AHZAB
34. SABA'
35. FATIR
36. YASIN
37. AS-SAFFAT
38. SAD
39. Al-ZUMAR
40. GHAFIR
41. FUSSILAT
42. AL-SHURA
43. AL-ZUKHRUF
44. AL-DUKHAN
45. AL-JATHIYAH
46. AL-AHQAF
47. MUHAMMAD
48. AL-FATH
49. AL-HUJURAT
50. QAF
51. AL-DARIYAT
52. AL-TUR
53. AL-NAJM
54. AL-QAMAR
55. AL-RAHMAN
56. AL-WAQI'AH
57. AL-HADID
58. AL-MUJADILAH
59. AL-HASHR
60. AL-MUMTAHANAH
61. AL-SAFF
62. AL-JUMU'AH
63. AL-MUNAFIQUN
64. AL-TAGHABUN
65. AT-TALAQ
66. AT-TAHRIM
67. AL-MULK
68. AL-QALAM
69. AL-HAQQAH
70. AL-MA'ARIJ
71. NUH
72. AL-JINN
73. AL-MUZZAMMIL
74. AL-MUDDATHTHIR
75. AL-QIYAMAH
76. AL-INSAN
77. AL-MURSALATE
78. AN-NABA'
79. AN-NAZI'AT
80. ABASA
81. AL-TAKWIR
82. AL-INFITAR
83. AL-MUTAFFIFIN
84. AL-INSHIQAQ
85. AL-BURUJ
86. AT-TARIQ
87. AL-A'LA
88. AL-GASHIYAH
89. AL-FAJR
90. AL-BALAD
91. AL-SHAMS
92. AL-LAYL
93. AL-DUHA
94. AL-SHARH
95. AT-TIN
96. AL-ALAQ
97. AL-QADR
98. AL-BAYYINAH
99. AL-ZALZALAH
100. AL-'ADIYAT
101. AL-QARI'AH
102. AT-TAKATHUR
103. AL-'ASR
104. AL-HUMAZAH
105. AL-FIL
106. QURAYSH
107. AL-MA'UN
108. AL-KAWTHAR
109. AL-KAFIRUN
110. AL-NASR
111. AL-MASAD
112. AL-IKHLAS
113. AL-FALAQ
114. AL-NAS